Thursday, July 11, 2013
KUANZISHA MKOA MPYA MBEYA NI KWA MASLAHI BINAFSI
Hivi karibuni imesikika kupitia kikao cha Ushauri cha mkoa (RCC) kupendekeza kuanzishwa kwa mkoa mpya kwa jina la songwe na kupendekeza makao makuu yake yawe mkwajuni huko chunya. kimsingi ktk zama hizi za mabadiliko makubwa ya kimfumo yayotaka kupeleka zaidi madaraka chini kwa wananchi (grassroot level), haya yanaainishwa vizuri zaidi katika reform ya serikali za mitaa, yenye nia mahususi ya kuona zana ya ushirikishwaji wa wananchi ktk kutumia rslimali walizonazo kuanzia ngazi za chini kabisa inapewa umuhimu mkubwa. kwa hali kama hii nadhani ingekuwa vema zaidi kama badala ya kuanzishwa kwa mkoa mpya basi ingekuwa bora kuanzishwa halmashauri katika wilaya kubwa kama chunya badala ya (Ku - Regionalize), tungali tukijua tatizo ni huduma kwa watu walio pembezoni halmashauri moja imekuwa vigumu kuifikia pande zote. hivyo tatizo la chunya kwa ukubwa wake si kweli kwamba Mh kandoro alikwama kuifikia bali huduma kupitia halmashauri ya chunya hazikuweza kupelekwa kutokana na ukubwa wa kijiografia.
Saturday, May 4, 2013
NINI UNGEKUWA MSIMAMO WAKO??
Mjumbe
wa Kamati Kuu ya Chama Cha demokrasia na Maendeleo (Chadema), Profesa
Mwesiga Beregu, amekataa kata kata wito wa chama chake wa kumtaka ajotoe
ndani ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba,huku yeye akiweka msimamo wake
wazi kwamba Tanzania ni muhimu zaidi kwake kuliko chama chake hicho.
Habari zilizoppatikana na kuthibitishwa Profesa Baregu, zinasema katibu Mkuu wa chama hicho Dk Wilbroad Slaa, alimwiita msomi ambae ni mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, akimtaka ajitoe. Ndani ya Tume hiyo kwasababu za kisiasa kwa madai kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeuteka mchakato huo.
Profesa Beregu anaelezwa kumjibu Dk Slaa kwa kutumia maneno ya kiingereza, "If I am told to choose between my country and my party (Chadema), I will choose my country", akiwa na maana kwamba kama angetakiwa kuchagua kimoja kati ya nchi yake na chama chake cha Chadema, angechagua nchi yake kwanza.
Akizungumza na Raia Mwema juzi Jumatatu jijini Dar es Salaam, Profesa Baregu amekiri kutoa msimamo huo Katibu Mkuu wake Dk Slaa, pamoja na chama chake cha Chadema, akisema viongozi wenzake hao wanapaswa kujishauri mara mbili mbili kabla ya kuchukua uamuzi huo wa kujitoa ikizingatiwa. Kwamba tangu mwanzo chama hicho ndicho kilichoasisi suala zima la Tanzania kuwa na Katiba Mpya tofauti na hii ya sasa.
Habari zilizoppatikana na kuthibitishwa Profesa Baregu, zinasema katibu Mkuu wa chama hicho Dk Wilbroad Slaa, alimwiita msomi ambae ni mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, akimtaka ajitoe. Ndani ya Tume hiyo kwasababu za kisiasa kwa madai kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeuteka mchakato huo.
Profesa Beregu anaelezwa kumjibu Dk Slaa kwa kutumia maneno ya kiingereza, "If I am told to choose between my country and my party (Chadema), I will choose my country", akiwa na maana kwamba kama angetakiwa kuchagua kimoja kati ya nchi yake na chama chake cha Chadema, angechagua nchi yake kwanza.
Akizungumza na Raia Mwema juzi Jumatatu jijini Dar es Salaam, Profesa Baregu amekiri kutoa msimamo huo Katibu Mkuu wake Dk Slaa, pamoja na chama chake cha Chadema, akisema viongozi wenzake hao wanapaswa kujishauri mara mbili mbili kabla ya kuchukua uamuzi huo wa kujitoa ikizingatiwa. Kwamba tangu mwanzo chama hicho ndicho kilichoasisi suala zima la Tanzania kuwa na Katiba Mpya tofauti na hii ya sasa.
Wednesday, May 1, 2013
MASHAKA S. MBUGI: FUKAMA ( FUNDISHA KADIRI YA MALIPO)
MASHAKA S. MBUGI: FUKAMA ( FUNDISHA KADIRI YA MALIPO): Walimu waonyesha kilio chao kwa kukubali yaishe, na hivyo kuja na kauli ya kuwataka walimu kufundisha kwa kadiri ya malipo wanayoyapata kwa ...
FUKAMA ( FUNDISHA KADIRI YA MALIPO)
Walimu waonyesha kilio chao kwa kukubali yaishe, na hivyo kuja na kauli ya kuwataka walimu kufundisha kwa kadiri ya malipo wanayoyapata kwa kifupi wanaita "FUKAMA" Hii imejitokeza kwa kuandika ujumbe huu katika mabango waliyoingia nayo katika maandamano ya Mei mosi Mbeya 2013 viwanja vya sokoine
Tuesday, April 30, 2013
MFUMO WA UENDESHAJI WA SERIKALI ZA MITAA NI CHANZO CHA USIMAMIZI MBOVU WA RASLIMALI
UWEPO WA SERIKALI ZA MITAA
Kwa mujibu wa sheria uwepo wa serikali za mitaa umeainishwa katika ibara ya 145 hadi 146 ya katiba ya jamhuri ya muungano wa tanzania ya mwaka 1977 na katika sheria za serikali za mitaa namba 7 ya mwaka 1982 kwa halmashauri za wilaya na sheria namba 8 ya mwaka 1982 kwa halmashauri za miji kwa maana ya manispaa na majiji sambamba na marekebisho yake ya mwaka 2002.
Kwa ufupi halmashauri zinaendeshwa kwa usimamizi wa karibu kupitia mabaraza ya madiwani ambao kimsingi utaratibu wa uendeshaji unaongozwa kanuni za madiwani za mwaka 2000 kwa halmashauri za miji. katika utaratibu huo unaweka wazi kuwa chombo chenye mamlaka ya juu ni baraza la madiwani yaani (full council) sambana na kamati ya fedha na uongozi inayohusisha wenyeviti wa kamati za kudumu kama kamati ya ujenzi na miundombinu, kamati ya Aridhi, mipango miji na mazingira na kamati ya elimu afya na uchumi.
kupitia utaratibu ulioainishwa kisheria unaotaka baraza la madiwani kuwa chombo cha juu chenye mamlaka ya usimamizi wa raslimali na uendeshaji wa halmashauri kumekuwepo na mapungufu makubwa yanayopelekea wajibu wa mabaraza (full council) kutokukidhi, moja ya kikwazo kikubwa ni mamlaka za uteuzi kwa watendaji wake akiwemo mkurugezi (mtendaji mkuu) ambaye kwa mujibu wa sheria anateuliwa na Rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania kwa halmashauri za miji na kwa upande wa halmashauri za wilaya huteuliwa na Waziri mkuu jambo ambalo linaleteleza utata katika uhusiano uliopo kiutendaji kwa misingi kwamba katika mazingira ya kawaida wakurugezi wengi wamekuwa wakitii zaidi mamlaka zilizowateua na kujikuta wakitekeleza maagizo tofauti na maazimio ya mabaraza yao, ipo mifano mingi lakini kwa ujumla wake hupelekea matumizi mabaya ya raslimali na hatimae migogoro isiyokwisha haswa ukizingatia kuwa wakurugenzi wengi wanajikuta wanawajibika kuwatumikia mabwana wawili na hatime kushindwa kuwa na misimamo makini. Pili lipo tatizo la uwajibikaji kwa dhana ya uwasilianaji (reporting system) kwa wakurugenzi wetu katika mazingira ya mwingiliano wa kisecta kwani upo wakati mkurugenzi anawajibika kutoa taarifa kwa vyombo vingine kama wizara ktk maana ya serikali kuu kwa utaratibu utakaokuwa umeainishwa na wizara husika kwa utarabu wa serikali kuu bila kuzingatia matakwa na uhitaji wa sheria inayosimamia serikali za mitaa kwa maana ya sheria ya fedha, na sheria mbali mbali ndogo zilitungwa kwa kuzingatia mazingira ya halmashauri husika.
Mapendekezo katika matatizo yanayojitokeza kwa halmashauri zetu ni kama ifuatavyo;
Mamlaka za uteuzi kwa halmashauri zetu zirudishwe kwa mabaraza husika kwa utaratibu wa ajira kwa ngazi za wakurugenzi serikali kuu itoe miongozo ya sifa na swala la uajiri liachwe kwa baraza la madiwani ambao ndiyo chomba simamizi kwa halmashuri. na kwa upana huu ni vema pia serikali ione uwezekano wa wenyeviti wa mabaraza haya kuchaguliwa na wananchi wote wa halmashauri husika badala ya sasa kuachiwa madiwani kufanya jukumu la kumpata mwenyekiti husika. kwa kufanya hivyo nina amini kuwa tutkuwa tumempunguzia Mh Rais mzingo mkubwa wa lawama anazozipata hivi sasa kutokana na uozo mkubwa miongoni mwa halmashauri zetu ikiwemo kutokuwachukulia hatua za kisheria kwa wakati wanapokuwa wameenenda tofauti na maadili ya kiutumishi. kumbuka kwa mfumo tulionao sasa hata kama chama chochote kikapata nafasi ya kuongoza nchi hii tatizo la usimamizi kwa halmashauri zetu likiwemo hili la uteuzi likibaki kuwa mikononi mwa chombo kingine nje ya chombo kinachosimamia kwa karibu halmashauri zetu.
Nitaendelea wiki ijayo
MASHAKA S. MBUGI: MANDHARI YA RUAHA NATIONAL PARK
MASHAKA S. MBUGI: MANDHARI YA RUAHA NATIONAL PARK: Twiga ni mnyama mpole na mtulivu na ndiyo maana amechukuliwa kama alama maalum ya nchi yetu katika maana nchi yenye amani na uvumilivu ...
MASHAKA S. MBUGI: UJIO WA RAIS MBEYA NAKUMBUKA ULE USEMI USEMAO MGEN...
MASHAKA S. MBUGI: UJIO WA RAIS MBEYA NAKUMBUKA ULE USEMI USEMAO MGEN...: Katika pitapita zangu siku mbili hizi yaani tarehe 28 na 29, nimeweza kuonana na ndugu na jamaa zangu wengi wao wakiwa katika pilikapilika ...
Monday, April 29, 2013
MANDHARI YA RUAHA NATIONAL PARK
Twiga ni mnyama mpole na mtulivu na ndiyo maana amechukuliwa kama alama maalum ya nchi yetu katika maana nchi yenye amani na uvumilivu
uvumilivu ni sifa pekee ya watanzania ingawa siku za hivi karibuni tunaona uvumilivu unapotea na dalili hizi tunaziona kama vile watu kushindana kihoja haipo tena, imebaki kutishiana kwa misingi ya kwenda kuandamana, tumeshuhudia vingozi wetu wawakilishi kutukana matusi bungeni, tumeshuhudia kiongozi kutetea maovu, maandamano kati ya kundi moja zidi ya lingine. kimsingi viongozi wetu wamekosa uvumilivu, wamenyimwa uzalendo, maslahi binafsi kama kuchoma lami nk
UJIO WA RAIS MBEYA NAKUMBUKA ULE USEMI USEMAO MGENI NJOO ........ WENYEJI TUPONE
Katika pitapita zangu siku mbili hizi yaani tarehe 28 na 29, nimeweza kuonana na ndugu na jamaa zangu wengi wao wakiwa katika pilikapilika za hapa na pale, na bahati nzuri nilijaliwa kuwauliza kilichojili na majibu yalikuwa hivi;
Mfanyabiashara wa nyumba ya kulala wageni " Kwa siku hizi mbili namshukuru Mungu kwani nimepata watega wa kutosha" na kwa mfanyabiashara wa mchele alicheka na kudai wateja kwa jana na leo wapo tofauti ktk maana hawasemi nipunguzie zaidi ya kusema nifungie vipeto vya debe tatu kwa watu watatu na kulipa bila kigugumizi" mwisho alieniacha hoi ni wa kitimoto aliyedai mzigo kwa sasa haupatikani na wadau ni wengi, nipotaka kujua wametoka wapi ghafla alijibu kwa mkato haelewi ila wanaonekana ni wageni wengi wao. ndipo nilipokumbuka usemi usemao "Mgeni njoo wenyeji tupone" ugeni mkubwa unaotarajia kuja kesho wa mh Rais na msafara wake kwa namna fulani imegeuka neema kwa waliojipanga vizuri kutumia fursa hiyo ukiachilia mbali kwa baadhi ya wasiutakia mema mkoa wetu kwa maslahi ya msingi kutokana na madai yao lakini yasiyozingatia haki ya upande mwingine na hivyo kuonekana ni binfsi zaidi. Nina hakika wafanyabiashara wakubwa na wadogo Mbeya wamepata wakati mgumu sana wa kuweka mambo yao sawa kwa mahitaji makubwa ya ghafla kutokana na uhitaji mkubwa wa huduma zao na hivyo kulazimika kuwapoteza wateja kwa mfano wageni kuwapeleka kulala uyole na hotel za mbalizi.
MASHAKA S. MBUGI: "MBEYA KWANZA VYAMA/ITIKADI BAADAYE"
MASHAKA S. MBUGI: "MBEYA KWANZA VYAMA/ITIKADI BAADAYE": Rai yangu kwa wapenda maendeleo wote wa mbeya mjini, muda umefika tunahitaji kuachana na siasa za makundi na mambo ya vyama na badala yake t...
Subscribe to:
Posts (Atom)